Thursday, August 15, 2019

Rais wa Afrika kusini akutana na R ais Magufuli ikulu ya Tanzania



Dar es Salaam. Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa amemtembelea Rais John Magufuli wa Tanzania katika Ikulu ya Dar es Salaam leo Alhamisi Agosti 15,2019.
Rais Ramaphosa ameongozana na mke wake, Dk Tshepo Motsepe ambao wamepokelewa na mwenyeji wao, Rais Magufuli na mkewe, Janeth katika viwanja vya Ikulu.
Mara baada ya kuwasili, Kiongozi huyo wa Afrika Kusini amepata heshima ya kupigiwa wimbo wa taifa na mizinga sanjari na kukagua gwaride maalum lililoandaliwa maalum kwa ajili yake. 
Kiongozi huyo aliwasili jana usiku Jumatano Agosti 14,2019 kwa ziara ya siku mbili kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo, John Magufuli ambapo baada ya ziara hiyo, Rais Ramaphosa atashiriki Mkutano wa 39 wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika nchini humo Agosti 17 na 18, 2019.
Baada ya kutoka Ikulu hiyo ya Tanzania, Rais Ramaphosa atakwenda ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNICC) kwenye Jukwaa la Biashara na kesho Ijumaa ya Agosti 16, 2019 saa 3 asubuhi, Rais Ramaphosa atatembelea kambi ya wapigania uhuru Mazimbu mkoani Morogoro.


No comments:

Post a Comment