Monday, August 19, 2019

Air Tanzania yatumika kumrudisha wazari mkuu wa Eswatini



Dar es Salaam. Waziri Mkuu wa Eswatini, Sibussiso Dhlamini ameondoka  jijini Dar es Salaam, Tanzania leo Jumatatu Agosti 19, 2019 kurejea katika nchi hiyo kwa kutumia ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL).
Ameondoka leo mchana na  ndege aina ya Airbus A220-300 kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) huku akisindikizwa na Waziri wa Maji, Profesa Makame Mbarawa.
Dhlamini alikuwa nchini Tanzania kuhudhuria mkutano wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) uliomalizika jana Jumapili.

No comments:

Post a Comment