
Nairobi, Kenya. Mkufunzi wa usalama nchini Kenya, Inayat Kassam ambaye aliwaokoa mamia ya watu waliokuwa wametekwa kwenye jengo la Westgate mwaka 2013, ameibuka kinara tena kwenye tukio lililotokea jana nchini humo.
Tukio hilo lilikuwa la kigaidi ambapo Wakenya zaidi ya 800 walidhibitiwa kwenye jengo la Hoteli ya Dustid2 lililopo River Side jijini Nairobi.
Jengo hilo lilizingirwa na magaidi wa kundi la Al shabaab ambao walivamia jioni na kuua watu 14 kwa mujibu wa Rais wa nchi hiyo, Uhuru Kenyatta.
Watumiaji wa mitandao ya kijamii nchini humo wamekuwa wakituma pongezi kwa Kassam ambaye alijitolea nguvu na maarifa kuwalinda na kuwaokoa watu kwenye mashambulizi hayo mawili.
Kassam ni raia wa nchi hiyo mwenye ujuzi wa kutumia silaha za moto na mkufunzi wa masuala ya usalama.
Mwaka 2013 alijitolea kuwaokoa watu ambao walinasa kwenye jengo la Westgate baada ya kuvamiwa na magaidi na kisha kuanza kushambulia ovyo katika maduka yaliyomo.
Kutokana na kujitoa kwake, Kassam ameendelea kujizolea umaarufu mitandaoni kutoka kwa Wakenya wakimsifu kwa ushujaa wake.
No comments:
Post a Comment