Tuesday, January 28, 2020

Virusi vya Corona vyaanza kusambaa duniani



Dar es Salaam. Baadhi ya nchi zimeanza kutoa taarifa za wahisiwa wa ugonjwa wa virusi vya Corona, wakati mamlaka za China zikisema watu 106 wamepoteza maisha na zaidi ya watu 4,000 wameambukizwa.
Taarifa hiyo iliyotolewa leo Jumanne, Januari 28, 2020 na mashirika mbalimbali duniani, inaeleza baadhi ya nchi za Afrika zimeshatoa taarifa za kupata wahisiwa huku Ivory Coast ikiwa na mwathirika wa ugonjwa huo.
Licha ya kwamba Wachina wengi walisafiri kwa ajili ya sherehe za mwaka mpya na sasa wapo katika ratiba za kurejea nchi mbalimbali wanazoishi.
Hata hivyo, Mamlaka za China tayari zimeweka katazo kali la kusafiri na miji mikubwa kadhaa imesitisha huduma ya usafirishaji wa umma ili kuzuia maambukizi zaidi, hata hivyo katazo hilo halijataja iwapo raia hao hawaruhusiwi kutoka nje ya nchi hiyo.
Idadi ya walioambukizwa kimataifa imeongezeka kukiwa na taarifa za maambukizi mapya huko Singapore na Ujerumani.
Marekani, ambayo ina maambukizi ya watu kadhaa, imewataka raia wake, ''kufikiria upya suala la kusafiri'' kwenda China na imeshauri kutosafiri kwenda Hubei.

No comments:

Post a Comment