Monday, September 21, 2020

Magufuli awapa maagizo mawaziri

 




RAIS John Magufuli ametoa maagizo kwa mawaziri watatu akitaka yatekelezwe haraka ili Wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma itoe huduma kwa ufanisi na kutatua kero za wananchi.

Mawaziri hao ni Seleman Jafo (Ofisi ya Rais – Tamisemi), Dk. Medard Kalemani (Nishati) na Inocent Bashungwa (Wizara ya Viwanda na Biashara).

Katika maagizo hayo, mawaziri hao wametakiwa kutekeleza kila mmoja kulingana na wigo wa wizara yake, huku wakiagizwa kuharakisha utekelezaji huo.

Rais Magufuli alitoa maagizo hayo jana akiwa njiani kuelekea mkoani Tabora akitokea Kigoma ambapo alisimama katika maeneo mbalimbali yakiwemo Kazuramimba, Uvinza, Mpeta, Nguruka, Kaliua na kuzungumza na wananchi.

Miongoni mwa changamoto kubwa katika maeneo hayo ni ubovu wa barabara, ukosefu wa umeme katika baadhi ya vijiji, maji na uendelezaji wa kiwanda cha chumvi cha Uvinza.

Akizungumza na wananchi katika kampeni za Uchaguzi Mkuu zinazoendelea, Rais Magufuli alisema hajaridhika na kasi ya usambazaji umeme katika wilaya hiyo na kuahidi kuwa vijiji 61 ambavyo bado havijapata umeme vitapelekewa.

“Naseme kwa uwazi kwamba suala la umeme katika vijiji na wilaya ya Uvinza hatujafanya vizuri sana, nitawabana watu wangu na waziri wangu wa umeme kama anasikia aanze kutekeleza kwa sababu bado ni waziri.

“Mheshimiwa Waziri Ndalichako (Elimu, Sayansi na Teknolojia) nataka ukamweleze Waziri Kalemani (Nishati) kwenye suala la umeme Uvinza sijafurahia, lakini nawaambia hivi vijiji 61 nitalibeba.

“Hatuwezi tukapeleka kwa miaka mitano vijiji 17 tu, tulitakiwa tuwe tumepeleka kwenye vijiji 61 vibaki 17 tu, hii ni kero lazima nibebe mimi mwenyewe,” alisema Rais Magufuli.

Kwenye miundombinu alisema barabara ya Uvinza – Malagarasi kilomita 150 itatengenezwa kwa kiwango cha lami na kwamba mwezi ujao zabuni itatangazwa.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli zaidi ya Sh bilioni 51 ambazo zinatarajiwa kutatumika katika ujenzi huo zimetolewa na Quwait Fund na Opec Fund.

Pia alisema katika barabara ya Uvinza – Mjini ambayo awali ilipangwa kutengenezwa kilimota moja, aliagiza ziongezwe kilometa nyingine 9 na kumtaka Waziri wa Nchi (Ofisi ya Rais – Tamisemi), Seleman Jafo kutafuta Sh bilioni 5 za ujenzi huo.

“Nataka siku moja nikija kuweka jiwe la msingi niikute lami mpaka Uvinza, natoa maagizo Jafo uwaletee bilioni tano kuanzia Jumatatu ziwe zimeshafika Uvinza,” alisema Rais Magufuli wakati akizungumza kwa njia ya simu na Jafo.

Aidha alimuagiza Waziri Bashungwa (Viwanda na Biashara) kufuatilia kiwanda cha chumvi ili kiweze kuendelezwa kuongeza fursa za ajira kwa vijana.

“Tuna kiwanda cha chumvi kikubwa sana tunataka tuki – promote kiwe kinauza mpaka Burundi, DRC na kwingine na vijana wetu wapate ajira, kwa hiyo, Waziri wa Viwanda naye hili akalibebe,” alisema.


Saturday, July 11, 2020

Uchaguzi wa Tanzania 2020: CCM yafanya Mkutano Mkuu kumpitisha Magufuli kuwania tena urais

Mkutano mkuu wa CCM
Maelefu ya wajumbe wa CCM wanakutana hii leo jijini Dodoma katika mkutano mkuu.
Pamoja na mambo mengine, wajumbe wa mkutano huo watamchagua ni mgombea urais yupi atakae peperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktaba mwaka huu.
Jina la rais John Magufuli ndilo litakalopitishwa baada ya Halmashauri Kuu Taifa kumpendekeza bila kupingwa hapo jana.
Humphrey Polepole
Maelezo ya picha,
Humphrey Polepole Katibu mwenezi wa CCM
Humphrey Polepole ambae ni Katibu mwenezi wa CCM amesema mkutano huo pia umehudhuriwa na wageni mbalimbali kutoka mataifa mengine ikiwemo viongozi wa vyama vya Ukombozi kutoka mataifa ya Afrika.
Dr Hussein Mwinyi tayari ametangazwa kuwa mgombea urais kupitia CCM Kwa upande wa Zanzibar.
Wawakilishi mbalimbali wahudhuria mkutano mkuu wa CCM
Maelezo ya picha,
Wawakilishi mbalimbali wahudhuria mkutano mkuu wa CCM
Baadhi ya nchi ambazo zimetuma wawakilishi wake katika mkutano wa leo ni pamoja na Vietnam, msumbuji, DRC, Burundi na Sudan Kusini.

Magufuli apitishwa kuwania awamu ya pili

Rais Magufuli wa Tanzania
Maelezo ya picha,
Rais Magufuli wa Tanzania
Kikao cha siku ya Ijumaa kilimpitisha kwa pamoja rais John Pombe Magufuli kuwania awamu ya pili ya urais wa Tanzania.
Magufuli hakuwa na mpinzani katika mchakato huo kwa kuwa hakukuwa na mwanachama mwingine wa CCM aliyejitokeza kugombea nafasi hiyo.
"Niwaombe wote tukashirikiane kutafute ushindi...wakati mwengine kunakuwa na hali ya kujiamini. Tukijiamini hatutashiriki ipasavyo, tukafanye kazi kwa nguvu ili tukapate ushindi wa kishindo," alisema Magufuli baada ya kupitishwa.
Kama ilivyo kwa jina la Mwinyi, jina la Magufuli linapelekwa kwenye Mkutano Mkuu wa CCM Taifa ili lithibitishwe rasmi.
Bado haijabainika upinzani utamchagua nani kupambana na Magufuli katika kinyang anyiro cha uchaguzi wa rais.
Ingawa Magufuli anasifiwa kwa kuanzisha miradi kadhaa, wakosoaji wake ikiwemo makundi ya haki za binadamu wanasemma ametumia nafasi yake kukandamiza upinzani na uhuru wa habari.

Monday, April 27, 2020

Aliyekuwa mbunge Mafia afariki dunia


ALIYEKUWA  Mbunge wa Mafia mkoani Pwani, Abdulkarim Shah amefariki dunia.
Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Taifa Gas, Rostam Aziz ilisema Shah alifariki juzi katika Hospitali ya Hindu Mandal.
“Hadi anafariki dunia Jumamosi, mheshimiwa Shah alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakarugenzi wa Taifa Gas,”alisema Rostam
Kuhusu taratibu za msiba na mazishi, alisema zitatangazwa baadaye, baada ya kukamilika taratibu zote.
Enzi za uhai wake,  Shaha  aliwahi kuwa mmoja wa makamishina wa Bunge na Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.
Alizaliwa eneo la Gerezani mwaka 1961 na kupata elimu msingi mwaka 1969 hadi 1975 katika Shule ya Msingi Muhimbili.
Baadae alipata elimu ya sekondari Shule ya Kinondoni mwaka 1976 na kuhitimu 1979.

Madereva 4 wa malori kutoka Tanzania wakutwa na virusi vya corona Uganda

Malori ya mizigo yanayoingia na kutoka Uganda
Wizara ya afya nchini Uganda imetangaza wagonjwa wanne wapya wa virusi vya corona na kufanya idadi ya wanaothirika na ugonjwa huo kufikia 79.
Wagonjwa hao wanne ni madereva wa malori kutoka Tanzania waliowasili nchini humo kupitia mpaka wa Mutukula.
Wagonjwa hao ni miongoni mwa sampuli 1,578 zilizochukuliwa kutoka kwa madereva wa malori.
Kati ya sampuli za wakaazi 411 zilizochukulia ili kufanyiwa vipimo hakuna hata mtu mmoja aliyekutwa na ugonjwa huo.
Hatua hiyo inajiri siku chache tu baada ya Uganda kuwarudisha nyumbani kwa lazima raia mmoja wa Tanzania na mwengine wa Kenya ambao walikutwa na virusi hivyo.
Uamuzi huo umedaiwa kuathiri uhusiano kati ya mataifa hayo wanachama wa Afrika mashariki na hivyobasi kuhatarisha usafirishaji wa mizigo kati yao.
Kufurushwa huko ambako ni kinyume na mwongozo wa shirika la Afya duniani WHO kuhusu jinsi ya kukabiliana na majanga kama vile Covid-19 pia, umeliweka katika ratili soko huru la Afrika mashariki.
Uganda imedaiwa kuwarudisha nyumbani kwa lazima dereva hao wa malori ambao walikutwa na virusi vya corona , huku jopo lililoundwa nchini Sudan Kusini kukabiliana na Covid-19 likiamua kuwafurusha Wakenya wawili kwa kutumia ndege kulingana na gazeti la The East African .
Dereva mwanamume mwenye umri wa miaka 27 alikutwa na virusi hivyo kati ya madereva 372.
Sampuli yake ilichukuliwa katika kituo cha kibiashara kilichopo mpakani cha Malaba na anatarajiwa kurudishwa nyumbani ili kupatiwa matibabu.

Idadi ya malori yanayoingia Uganda kwa siku

Huku takriban malori 1000 ya mizigo yakidaiwa kuingia katika taifa hilo kwa siku, Madareva wa malori ya masafa marefu wamekuwa wasiwasi mkubwa nchini Uganda baada ya kuthibitishwa kuwa chanzo kikuu cha ugonja huo miongoni mwa raia wa kigeni.
Kati ya visa vipya vya Covid vilivyotangazwa nchini Uganda siku ya Ijumaa, wagonjwa sita walikuwa madereva wa malori kutoka Tanzania waliowasili kupitia mpaka wa Mutukula huku madereva wengine watano wakidaiwa kutoka Kenya waliongia kupitia mpaka wa Malaba na Busia.
Idara ya Afya nchini Uganda inayosaidiwa na vikosi vya usalama imedaiwa kumsaka dereva wa lori wa Tanzania ili kumrudisha nyumbani kwa matibabu.
Tukio jingine ni la dereva mwengine wa malori raia wa Tanzania mwenye umri wa miaka 34 kutoka Dar es Salaam ambaye aliwasili katika mpaka wa Mutukula tarehe 16 Aprili na ambaye hakuonyesha dalili zozote za Covid-19.
Kenya imekuwa ikiwatibu baadhi ya raia wa kigeni wanaokutwa na virusi hivyo kulingana na kaimu mkurugenzi wa huduma ya afya Dkt Patrick Amoth.
''Tumewatibu wagonjwa wengi wa mataifa ya kigeni kutoka Cameroon, Pakistan, Burundi na DRC . Kama taifa hatujaona sababu ya kuwatimua kutokana na hatari zinazohusishwa na usafiri wakati mtu anapougua virusi hivyo'', alisema Dkt. Amoth.
''Inashangaza mtu kufanya uamuzi kama huo kwasababu unaweza kuwaambukiza watu wengi zaidi unapomruhusu muathiriwa wa virusi vya corona kusafiri mbali wakati ambapo ingekuwa bora kumtibu katika taifa alilokutwa na virusi hivyo''. Aliongezea.
Museveni amesema baada ya kushughulikia ipasavyo mipaka ya anga, sasa hatua inayofuata ni kushughulikia pia mipaka ya ardhini na nchi jirani ili kuendelea kuzuia kasi ya maambukizi.
Maafisa waandamizi wa serikali ya Uganda wamekuwa wakinukuliwa kuwa wanataka madereva kutoka Kenya na Tanzania kuacha magari mpakani.
Baada ya kuyaacha hapo yatachukuliwa na madereva wa Uganda ambao watayapeleka mpaka mwisho wa safari. Museveni amethibitisha mpango huo akisema mawaziri wa afya wanaujadili
"Kubadili madereva, Madreva kutoka Kenya waendeshe mpaka mpakani kisha magari kupulizwa dawa na madereva wengine (wa Uganda) kuyachukua kutokea hapo. Hili pia mawaziri watalijadili," ameema Museveni.
Pia Uganda inataka madereva hao kupimwa kabla ya kutoka katika nchi zao.
Hatua nyengine ambayo Uganda inapanga kuitekeleza kwa sasa ni kuhakikisha wanawapima madereva wote kutoka nchi jirani na kuwaruhusu kuendelea na safari pale tu majibu yatakapotoka na kuonesha hawana maambukizi.
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uganda Jenerali Jeje Odongo aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali ilikuwa inapanga kutumia vipimo vya haraka kuwapima madereva hao.
"Vipimo vya haraka vinatumia dakika 10 tu kutoa majibu, lakini changamoto yake ni kuwa kipimo kimoja ni dola 65 na kwa wastani siku moja magari 1,000 huingia Uganda.

Amri ya kutoka nje Uganda

Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametagaza masharti zaidi ya kukabiliana na kuenea kwa virusi vya corona wiki mbili baada ya kupiga marufuku usafiri wa Umma.
Katika hotuba yake kwa taifa iliyopeperushwa moja kwa moja kwenye televisheni Bw. Museveni alipiga marufuku usafiri wa kutumia magari binafsi na boda boda kuanzia saa nne usiku.
Mtu yeyote anayehitaji huduma za dharura za kiafya kama vile kujifungua au kufanyiwa upasuaji anatakiwa kupata idhini kutoka kwa maafisa wa serikali katika ngazi ya Wilaya kabla ya kutoka nyumbani
Wauzaji bidhaa za chakula sokoni watahitajika kuondoka maeneo yao ya biashara hadi pale serikali itakapokamilisha kushughulikia maeneo mapya ya wao kuuzia bidhaa zao .
Rais Museveni pia ameahidi msaada wa chakula kwa watu ambao hawafanyi kazi kutokana na vikwazo vya kukabiliana na covid-19 na hawana uwezo wa kujipatia bidhaa hiyo muhimu.

Friday, April 24, 2020

Wanasayansi wa Uingereza wanataka chanjo yao ya corona kufanyiwa majaribio Kenya

vaccine
Watafiti kutoka nchini Uingereza wanafikiria kufanyia majaribio chanjo ya virusi vya corona nchini Kenya ambapo kulingana na wao mlipuko wa ugonjwa huo unaongezeka.
Hatua hiyo inajiri wiki moja baada ya Shirika la Afya duniani kuyaonya mataifa ya Ulaya kwamba bara la Afrika sio uwanja wa majaribio ya chanjo.
Mkuu wa Shirika hilo Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus alilaani kauli alizoziita za "kibaguzi" kutoka kwa madaktari wawili wa Ufaransa ambao walitaka chanjo ya virusi vya corona kufanyiwa majaribio barani Afrika.
"Afrika sio na haitakuwa uwanja wa majaribio ya chanjo yoyote," alisema Mkurugenzi Mkuu wa WHO Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus.
Mkuu wa shirika la Afya Duniani Dkt Tedros Adhanom Ghebreyes amesema kwamba bara la Afrika halitakuwa uwanja wa majaribio ya chanjo ya corona
Image captionMkuu wa shirika la Afya Duniani Dkt Tedros Adhanom Ghebreyes amesema kwamba bara la Afrika halitakuwa uwanja wa majaribio ya chanjo ya corona
Hatahivyo wanasayansi hao kutoka Chuo kikuu cha Oxford wanadaiwa kufikiria wazo hilo iwapo hawatopata matokeo ya haraka nchini Uingereza.
Chanjo hiyo inajulikana kutoa antobody yenye nguvu, lakini hilo halimaanishi kwamba inaweza kuwa kinga.
''Tutalazimika kuhitaji chanjo chungu nzima , kuna nyingi zinazofanyiwa majaribio hivyobasi tutahitaji dozi nyingi na tutarajie mjadala mkubwa kuhusu ni mataifa gani ama ni kundi lipi la watu linalohitaji chanjo hiyo kwanza'', alisema mwandishi wa BBC wa maswala ya tiba Fergus Walsh.
Alikuwa akizungumza katika runinga ya BBC News ambapo mtangazaji Sophie Raworth alimtaka kutoa mtazamo wake kuhusu ufanisi wa chanjo hiyo.
Walsh alijibu akisema kuna umuhimu kuwa makini na ahadi zinazotolewa kutokana na kile alichokitaja kuwa hamu ya chanjo hiyo kufanya kazi.
Hatahivyo, kulingana na Walsh, kundi hilo la Oxford lina rekodi nzuri ya kipindi cha miaka 30 iliopita ambapo limefanikiwa kutengeneza chanjo zilizofanikiwa dhidi ya aina nyengine ya virusi vya corona kama vile MERS, ambayo imefanikiwa katika majaribio yaliofanyiwa katika miili ya binadamu.
Hatahivyo kuna maswali kuhusu uamuzi wa kufanyia majaribio chanjo hiyo nchini Kenya licha ya wagonjwa wachache wa virusi hivyo kuripotiwa nchini humo.
Kufikia Alhamisi tarehe 23 Aprili, kulikuwa na wagonjwa 320 walioripotiwa katika taifa hilo la Afrika mashariki.
Mapema siku ya Alhamisi, majaribio ya kwanza katika mwili wa mwanadamu barani Ulaya yalianza Oxford katika kile ambacho vyombo vya habari vya Uingereza vimetaja kuwa wakati muhimu.

Watu wawili waliojitolea, wote wakiwa wanasayansi walichomwa sindano ya chanjo na ndio watu wa kwanza kati ya zaidi ya watu 800 walio kati ya umri wa miaka 18 hadi 55 ambao walichaguliwa kufanyiwa utafiti huo.

Mtu wa kwanza kujitolea alitambulika kuwa mwanasayansi kwa jina Elisa Granato aliye katika idara ya wanyama katika chuo kikuu cha Oxford.

''Mimi ni mwanasayansi na nataka kusaidia sayansi, kwa uwezo wangu wote na kwasababu sifanyi utafiti wa virusi, nilihisi hii ndio jinsi ninavyoweza kusaidia katika utafiti huu. Ndio maana niko hapa na nafurahia'', alimwambia Walsh.
Nusu ya kundi hilo litapokea chanjo ya Covid 19 huku nusu nynegine ikipokea chanjo ya udhibiti ambayo inalinda dhidi ya ugonjwa wa menenitis lakini matokeo yake hayatajulikana kwa miezi kadhaa.

Katika mjadala kwenye runinga ya ufaransa ya channel LCI, Dkt Camille Locht, mkuu wa utafiti kutoka shirika la utafiti wa afya la Inserm alikuwa akiongelea juu ya majaribio ya chanjo barani Ulaya na Australia.

Dkt Jean-Paul Mira,mkuu wa kitengo cha wagonjwa mahututi katika hospitali ya Cochin ya jijini Paris, kisha akasema: "Nichokoze kitu, siyo kwamba tunatakiwa kufanya utafiti huu Afrika, ambako hakuna barakoa, hakuna matibabu wala huduma ya nusu kaputi?
Huku hayo yakijiri, dawa iliyokuwa ikitazamiwa kutibu virusi vya corona inaripotiwa kushindwa kufikia viwango vya ufanisi katika jaribio la kwanza la matibabu.

Kumekuwa na matumaini makubwa kwamba dawa ya remdesivir ingeweza kutibu ugonjwa wa virusi vya corona, Covid-19.

Lakini jaribio la dawa hiyo nchini Uchina limeonesha kuwa dawa hiyo haikufanikiwa, kwa mujibu wa waraka uliochapishwa kimakosa na Shirika la Afya Duniani (WHO).
Dawa hiyo haikuboresha hali za wagonjwa au kupunguza kiwango cha virusi katika damu, ulisema waraka huo.
Kampuni ya Marekani inayotengeneza dawa hiyo, Gilead Sciences, imesema kuwa waraka huo ulipotosha uchunguzi wake.

Mkuu wa WHO Afrika akosoa kasi ya Tanzania kuchukua tahadhari

mAGUFULI
Kuchelewa kwa Tanzania kuchukua hatua kali za kukabiliana na kusambaa kwa maambukizi ya corona kunatajwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) kama sababu ya kuongezeka kwa wagonjwa nchini humo.
Mkuu wa WHO wa bara la Afrika Bi Matshidiso Moeti anasema kuwa kumekuwa na hofu juu ya kukua kwa kasi ya maambukizi katika taifa hilo la Afrika Mashariki.
"Kwa hakika tumeona kuwa watu kuaacha kuchangamana, pamoja na kupiga marufuku kwa mikusanyiko ya watu wengi kumechukua muda mrefu kufanyika na tunaamini kuwa hayo yanaweza kuwa ni moja ya mabo yaliyopelekea ongezeko la kasi la wagonjwa wa corona," ameeleza Dkt Moeti katika mkutano na wanahabari.
Tanzania kwa mara ya kwanza iliripoti mgonjwa wa kwanza wa corona Machi 16 na kufikia sasa idadi ya maambukizi imefikia 284.
Baada tu ya kuripotiwa kwa ugonjwa huo, serikali ya Tanzania ilitangaza kufungwa kwa shule na vyuo vikuu pamoja na matukio ya kukusanya watu wengi kama ligi za michezo ikiwemo mpira na matamasha ya muziki.
Hata hivyo, serikali ya rais John Pombe Magufuli imekosolea vikali kwa kutochukua hatua kali kama kufunga (lockdown) vitovu vya maambukizi kama miji ya Dar es Salaam na Zanzibar.

Jumatano, rais wa Tanzania John Pombe Magufuli liweka wazi kuwa serikali yake haitalifungia jiji la Dar es Salaam.

Licha ya Dar es Salaam kuwa kitovu cha maambukizi, Magufuli amesema jiji hilo la watu milioni sita ndio moyo wa mapato ya Tanzania.
"Wapo wengine wanatoa mawazo ya kuifunga Dar es Salaam, hili haliwezekani. Dar es salam ndio centre (sehemu) pekee ambapo collection (makusanyo) ya revenue (mapato) inapatikana kwa nchi yetu...Zaidi ya asilimia 80 ya mapato yanakusanywa Dar es Salaam," alisema Magufuli alipokutana na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama vya nchi hiyo Jumatano.
Pia alisisitiza kuwa kutokana na wingi wa wakaazi wake, ilikuwa ni jambo la kutegemewa kitakwimu kwa jiji hilo kuwa na wagonjwa wengi zaidi.
Awali asubuhi ya siku hiyo hiyo, Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Kassim Majaliwa akiongea kwenye ibada ya kuiombea nchini hiyo alisema anatambua kwamba kuna Watanzania ambao wanataka serikali ichukue hatua nyingi zaidi kudhibiti maambukizi ya virusi, lakini ameonya kuwa kila hatua ina faida na hasara zake.
"Ni vyema wajue kila hatua ina faida na hasara zake...Serikali inaendelea kutathmini kila hatua kwa faida na hasara zake kwa jamii. Ni vyema Watanzania mkaendelea kuiamini serikali, kuwaamini wataalamu wetu katika kuchukua hatua ambazo haziwezi kuleta athari zaidi kwa taifa."

Hatuazilizochukuliwa kudhibiti maambukizi ni 

  • Shule zote na vyuo vya elimu vimefungwa mpaka itakapotangazwa ili kuzuia kuenea kwa maambukizi ya corona nchini humo.
  • Pamoja na kuzuia mikusanyiko yote ya watu wengi yakiwemo matamasha ya muziki, mikutano ya hadhara mbalimbali ikiwemo ya kisiasa.
  • Magari ya usafiri wa umma hatayakiwi kujaza abiria, na wote lazima wawe wameketi vitini.
  • Ndege za abiria zimezuiwa kutua nchini humo.
  • Kuanzia Jumatatu ya Aprili 20 ni lazima kwa wakaazi wote wa Dar es Salaam kuvaa barakoa wanapokuwa maeneo ya umma.
  • Biashara zote za chakula jijini Dar es Salaam zinatakiwa kufunga bidhaa zao na kutoruhusu watu kula kwenye migahawa.

Wizara ya Mambo ya Ndani yamwaga ajira


DODOMA.  WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi imewasilisha bajeti ya mwaka 2020/21 ya zaidi ya Sh bilioni 899, huku ikimwaga zaidi ya ajira 4,000 kwa Jeshi la Magereza, Uhamiaji, Polisi, Zimamoto na Uokoaji.
Akiwasilisha bajeti hiyo bungeni jana, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, alisema kati ya ajira hizo 2,725 ni za Polisi, Uhamiaji 495, Magereza 685 na Zimamoto na Uokoaji 501.
Alisema Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na wadau wa ndani na nje ya nchi, pia limepanga kuendelea kutoa mafunzo kwa maofisa, wakaguzi na askari 9,465 na watumishi raia 25.
“Katika mafunzo hayo, maofisa 9,051 watapata mafunzo ndani ya nchi kupitia vyuo vya polisi na 414 nje ya nchi kwa udhamini wa taasisi na nchi mbalimbali,” alisema Simbachawene.
 Alisema katika mwaka 2020/21 Idara ya Uhamiaji inatarajia kuajiri askari 495 na kuwapa mafunzo ya awali.
Pia, itaendelea kutoa mafunzo mbalimbali kwa maofisa, askari na watumishi raia ili kuwaongezea ujuzi wa utendaji kazi kwa ufanisi zaidi.
Simbachawene alisema katika kukabiliana na changamoto ya upungufu wa rasilimali watu, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linatarajia kuwapandisha vyeo maofisa na askari 1,311 na kuajiri askari wapya 501 katika mwaka 2020/21.
“Askari hao watakaoajiriwa watapatiwa mafunzo ya awali ya kuzima moto na uokoji katika Chuo cha Zimamoto na Uokoaji kilichopo Chogo (Handeni) mkoani Tanga,” alisema Simbachawene.
Kuhusu mafunzo na ajira kwa watumishi wa Jeshi la Magereza, alisema katika kipindi cha Julai, 2019 hadi Machi, 2020 maofisa na askari 1,537 walipata mafunzo ya uongozi wa kijeshi katika vyuo vya Magereza na watumishi 951 walihitimu mafunzo ya taaluma mbalimbali katika vyuo vya ndani na nje ya jeshi.
”Jeshi linatarajia kuajiri askari 685 wenye fani mbalimbali watakaopatiwa mafunzo ya awali katika Chuo cha Magereza Kiwira (Mbeya),” alisema Simbachawene.
Alisema pia jeshi hilo linatarajia kutoa mafunzo ya uendeshaji wa magereza na taaluma ya urekebishaji kwa maofisa na askari 3,270 katika ngazi mbalimbali za uongozi.
BAJETI YAPUNGUA 
Katika mwaka wa fedha 2019/20, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliidhinishiwa bajeti ya Sh 921,247,033,279 na kati ya fedha hizo, Sh 517,040,341,000 ni kwa ajili ya mishahara, Sh 372,268,278,000 matumizi mengineyo na Sh 31,938,414,279 miradi ya maendeleo.

Thursday, April 23, 2020

Rais wa Madagascar adai kupata tiba ya corona

President Andry Rajoelina attends a ceremony to launch Covid Organics in Antananarivo - 20 April 2020
Wakati wanasayansi duniani wakihangaika kupata chanjo na tiba ya virusi vya corona, rais wa Madagascar Andry Rajoelina amezindua dawa ya mitishamba ''inayotibu'' Covid-19 .
Hata hivyo Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema kuwa hakuna ushahidi wa tiba ya Covid-19 baada ya Bwana Rajoelina kutangaza dawa yake.
Taasisi ya taifa ya tiba nchini Madagascar (Anamem) pia imeonyesha wasiwasi wake juu ya ufanisi wa dawa hiyo inayoelezewa na rais Andry Rajoelina kama yenye uwezo wa kuzuwia na kupona corona.
Taasisi hiyo imesema kuwa mitishamba inaweza kudhuru afya ya mtu kwani "hakuna ushahidi wa ufanisi wake kisayansi".
Mmea huo unatarajiwa kutolewa bure kwa watu wenye uwezekano mkubwa wa kuathiriwa na na virusi vya corona.
Ikizinduliwa kwa jina Covid-Organics, dawa hiyo imetengenezwa kutoka kwa mmea artemisia (pakanga)-ambao ni mojawapo ya miti ambayo huchanganywa pamoja na mimea mingine ya Madagascar kama tiba ya ugonjwa wa Malaria.
Dawa hiyo ambayo imepakiwa kwenye chupa na kutangazwa kama chai ya miti shamba baada ya kujaribiwa kwa watu chini ya 20 kwa kipindi cha wiki tatu, katibu wa rais Lova Hasinirina Ranoromaro ameiambia BBC.
Bottles of Covid-OrganicsHaki miliki ya pichaAFP
Image caption
"Vipimo vimefanyika-watu wawili wamekwishapona kutokana na tiba hii," Bwana Rajoelina alisema katika uzinduzi wa Covid-Organics uliofanyika katika taasisi ya utafiti ya Madagascar- Malagasy Institute of Applied Research (Imra), abayo ndiyo iliyotengeneza dawa hiyo ya mitishamba.
"Kinywaji cha dawa hii ya mitishamba huonesha matokeo katika kipindi siku saba," alisema rais huyo mwenye umri wa miaka 45, ambaye aliwataka watu kuitumia kama hatua ya kujikinga na ugonjwa wa corona.
"Watoto wa shule wanapaswa kupewa kinywaji ... kidogo kidogo kwa siku nzima," aliwaambia mabalozi na watu wengine waliokua wamekusanyika kwa ajili ya uzinduzi wa kinywaji hicho.
Dkt Charles Andrianjara, Mkurugenzi mkuu wa taasisi ya utafiti ya Imra, anaafiki kuwa Covid-Organics inapaswa kutumiwa kama kinga.
Lakini alijihadhari zaidi kuzungumzia zaidi juu ya matumizi ya dawa hiyo kama tiba, lakini akasema kwamba uchunguzi wa kimatibabu umeonyesha "dalili ya ufanisi wake kama tiba", shirika la habari la AFP lilimnukuu akisema.
Kisiwa hicho cha Bahari ya Hindi kimekwisharekodi hadi sasa wagonjwa 121 wa virusi vya corona, na hakuna vifo kutokana na ugonjwa huo.

Ikizungungumzia uzinduzi wa Covid-Organics, WHO imeambia BBC kwamba shirika hilo la dunia halishauri "matibabu ya kibinafsi ya dawa zozote... kama njia ya kinga au tiba ya Covid-19."

Lilirejelea kauli za mkuu wa WHO Tedros Adhanom Ghebreyesus kwamba "hakuna njia za mkato" za kutafuta dawa ya kupambana na virusi vya corona.

Majaribio ya kimataifa yanaendelea kupata tiba yenye ufanisi , WHO iliongeza.Bi Ranoromaro alisema kuwa rais Rajoelina anatambua kuwa WHO lazima izingatie utaratibu wake lakini akasema kuna suala la uhuru na mamlaka ya taifa kujifanyia mambo yake.
"Ana wajibu kwa watu wa Madagascar," alisema.
'Madhara makubwa'
Profesa Brian Klaas, mtaalamu wa Madagascar katika Chuo cha London, amesema kuwa msimamo wa Bwana Rajoelina unaweza kusawasababishia Wamadagascar madhara kuliko mema.
"Ni hatari kwa sababu mbili-moja ni kwamba baadhi ya watu ambao hawapaswi kutumia kinywaji hicho watakitumia," aliimbia BBC.
"Na pili hilo litawapa watu dhana potofu ya kinga, kwa hivyo wataishia kufanya vitu ambavyo wasingevifanya kama dawa hiyo isingekuwepo na kujiweka na kuwaweka wengine hatarini."
Kama virusi vilishaanza kusambaa, inaweza kuwa jambo "baya" wakati mfumo wa huduma za afya wan chi ni dhaifu, ikizingatiwa kuwa nchi ina mashine za kusaidia kupumua(ventileta) sita tu kwa watu milioni 27, alisema.
"Pia ni mojawapo ya sababu kisiwa hicho ni moja ya maeneo duniani yenye milipuko ya magonjwa yanayosababishwa na bakteria ambao tayari huponywa na dawa sahihi."
Mwezi Machi, Kituo cha afya cha taifa cha Marekani - National Center for Complementary and Integrative Health kilionya juu ya matumizi ya dawa zinazodaiwa kutibu virusi vya corona, ikiwemo mitishamba na aina mbalimbali za chai-ikisema kuwa njia bora zaidi ya kuzuwia maambukizi ni kuepuka kujiweka katika hatari ya kupata virusi.

Tuesday, April 21, 2020

Virusi vya Corona: Wagonjwa wapya 15 wathibitishwa Kenya jumla kuwa 296

Dkt Mercy Mwangangi
Wizara ya Afya nchini Kenya imetangaza ongezeko la wagonjwa 15 wapya waliothibitishwa kuwa na virusi vya corona na kufikisha 296 jumla ya watu wanaougua Covid-19 nchini humo.
Wagonjwa 11 ni raia wa Kenya na wanne ni raia wa kigeni ambao walikuwa miongoni mwa watu 545 waliofanyiwa vipimo vya kubaini ikiwa wana virusi vya ugonjwa huo katika kipindi cha saa 24 zilizopita.
Akizungumza na wanahabari Jumanne, Katibu mkuu wa wizara hiyo Dkt. Mercy Mwangangi amesema visa saba vya maambukizi vilirekodiwa Mombasa pwani ya Kenya, sita mjini Nairobi na viwili katika mji wa kaskazini mashariki wa Mandera..
''Hakuna hata mmoja kati yao aliyekuwa na amesafiri'' alisema na kuongeza kuwa watu sita kati yao walikuwa karantini na wengine tisa walipatikana kupitia mkakati wa serikali wa kuwatafuta watu wanaoshukiwa kuambukizwa baada ya kutangamana na watu waliathirika.
Dkt. Mwangangi apia alitangaza kuwa watu watano zaidi wametolewa hospitali baada ya kupona na kuongeza idadi ya watu waliopona kutokana na virusi vya corona kufikia 74.
Wizara ya Afya pia imezindua kampeini kwa jina 'Saa sita'.
Wakenya wameombwa kuungana kuwapa pongezi wahudumuwa afya kila siku ya Jumatano "saa sita''.

Virusi vya Corona: Simulizi ya muuguzi ambaye hushuhudia saa za mwisho za wagonjwa wa corona

Nurse by a bed in a ICU
Kupata huduma ya mashine ya kusaidia upumuaji (Ventileta) inaweza kumaanisha tofauti kati ya maisha na kifo kwa wagonjwa walio mahututi kutokana navirusi vya corona. Lakini wakati mwingine hata mashine hizi za kupumua haziwezi kuokoa maisha ya mtu.
Kuzima mashine hizi ni sehemu ya majukumu ya Juanita Nittla.
Yeye ni Muuguzi mkuu kwenye kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali ya Royal Free jijini London, na amekuwa akifanya kazi katika hospitali ya taifa kama mtaalamu wa huduma kwa wagonjwa mahututi kwa kipindi cha miaka 16 iliyopita.
Kazi hii inatesa mno kisaikolojia inaumiza mno, anasema mhudumu huyu mwenye miaka 42. ''Wakati mwingine ninahisi kama nahusika na kifo cha mtu.''
Mashine za upumuaji huchukua nafasi ya mfumo mzima wa upumuaji wa mwanadamu iwapo virusi vya corona vitasababisha mapafu kushindwa kufanya kazi. Mashine hii humpa mgonjwa nafasi ya kupambana na maambukizi, lakini wakati mwingine mashine hii haitoshi.
Jopo la matabibu hukabiliana na uamuzi mgumu kuhusu muda wa kusitisha kazi ya mashine hiyo kwa wagonjwa ambao hawapati nafuu. Uamuzi hufikiwa baada ya kufanya uchunguzi wa kujiridhisha, kutathimini sababu mbalimbali kama vile umri wa mgonjwa, maradhi mengine ya muda mrefu waliyonayo jinsi wanavyopambana na virusi na uwezekano wao wa kupona.

Juanita Nittla in the ICU where she worksHaki miliki ya pichaJUANITA NITTLA
Image captionKuzima mashine ya ventileta ni sehemu ya majukumu ya Juanita Nittla.

Mwanzo wa zamu ya alfajiri katika wiki ya pili ya mwezi Aprili, Bi Nittla aliambiwa na msimamizi wa ICU kuwa kazi yake ya kwanza itakuwa kusitisha tiba kwa muuguzi mwenye miaka 50 aliyeathirika na virusi vya corona
Vikwazo vilivyokuwepo wakati huo ilimaanisha kuwa alipaswa kuzungumza na binti wa mgonjwa huyo kwa njia ya simu kumueleza kitakachotokea (kwa kuwaWaziri wa Afya nchini humo, Matt Hancock alisema kuwa ndugu wa karibu na familia watakuwa na nafasi ya kushuhudia na kumuaga ndugu yao kabla ya kuaga dunia, maelekezo mapya kuhusu wagonjwa wa corona walio katika hali mbaya)
''Nilimhakikishia tena kuwa mama yake hakuwa katika maumivu na alionekana kuwa sawa,'' Bi Nittla alisema. ''pia nilimuuliza kuhusu matakwa ya mama yake na hitaji la imani yake ya dini.''
Mgonjwa wa Bi Nittla alikuwa katika eneo la vyumba vinane, alizungukwa na watu ambao pia walikuwa hawajitambui.
"Nilifunga mapazia na kuzima kengele zote."
Timu ya matabibu ilisimama kwa muda na wakaacha kuongea, na Bi Nittla akaweka simu karibu na sikio la mgonjwa, na akamuomba binti yake azungumze.

A patient getting ventilator supportHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionVentileta - mashine iliyopo kushoto mwa picha - husaidia wagonjwa mahututi kupumua

Bi Nittla alipiga muziki ambao familia iliomba. Kisha akazima mashine.
''Nilikaa pembeni yake, nikiwa pembeni yake nimeshika mikono yake mpaka alipofariki,'' alisema.
Mgonjwa alifariki katika kipindi si chini ya dakika tano baada ya Bi Nittla kuzima mashine ya kumsaidia kupumua.
''Nilitazama taa za mashine zikiwaka na mapigo ya moyo yakionekana kwenye mashine yakigonga alama sifuri kwenye skrini,'' alisema. Bi Nittla aliondoa mipira iliyokuwa ikimpatia dawa mgonjwa.
Binti wa mgonjwa bado alikuwa akizungumza na mama yake akisali kwenye simu. Bi Nittla alinyanyua simu kumwambia kuwa sasa basi imekwisha.
''Kwa msaada wa mfanyakazi mwenzangu, nilimsafisha na kumfunga kisha kumuhifadhi kwenye mfuko maalum wa kuhifadhia miili. Niliweka ishara ya msalaba kwenye paji lake la uso kabla ya kuufunga mfuko,'' alisema.
Bi Nittla anasema kuwa kuweza kushughulika na watu walio katika hali ya kufa kumemsaidia sana kuweza kuendelea kulichukulia kawaida janga hili.
Kutokana na idadi kubwa ya watu wanaofika kulazwa, kitengo cha wagonjwa mahututi kimepanuliwa kutoka vitanda 34 mpaka vitanda 60.

'' Kwa kawaida katika kitengo hiki huwa kuna utaratibu wa muuguzi mmoja kushughulika na mgonjwa mmoja. Sasa imekuwa muuguzi mmoja kwa kila wagonjwa watatu,'' anasema Bi Nittla.
''Ikiwa hali itaendelea kuwa mbaya, itakuwa muuguzi mmoja kwa kila wagonjwa sita.''
Baadhi ya wauguzi katika jopo lake wameonesha dalili ya kuwa na maambukizi na sasa wamejitenga.
Hospitali inawafunza wauguzi wengine ili waweze kufanya kazi katika kitengo cha wagonjwa mahututi.
''Kabla ya kuanza zamu huwa tunashikana mikono na kusema'baki salama'. Huwa tunalindana wenyewe kwa wenyewe. Tunahakikisha kila mmoja wetu anavaa glovu, barakoa na vifaa vya kujikinga vyema,'' anasema Nittla.

Nurses in protective equipment before the start of the shiftHaki miliki ya pichaJUANITA NITTLA
Image captionBi Nittla anasema wauguzi wa ICU hujumuika pamoja na kutakiana kheri kabla ya kuanza kwa zamu

ICU hurekodi kifo kimoja kila siku, juu ya wastani waliokuwa wakirekodi kabla ya janga la corona.
''Inatisha ,'' anasema Bi Nittla.Kama muuguzi mkuu, wakati mwingine analazimika kuondoa hofu aliyonayo.
''Ninapata ndoto .Ninashindwa kulala.Nina hofu kuwa nitapata maambukizi.Kila mmoja ana hofu.''
Mwaka jana hakuwa kazini kwa miezi kadhaa baada ya kupata kifua kikuu. Anafahamu kuwa uwezo wake wa mapafu umedhoofu.
''Watu huniambia sitakiwi kufanya kazi lakini hili ni janga.Ninaacha kila kitu kando na kufanya kazi yangu,'' anasema.
''Mwishoni mwa zamu yangu ya siku huwa ninawaza wagonjwa waliofariki wakiwa chini ya uangalizi wangu, lakini huwa nafuta mawazo hayo ninapotoka nje ya jingo la hospitali.''
Tangu alipozungumza na BBC, Bi Nittla ametakiwa na mwajiri wake kubaki nyumbani, kutokana na hali yake ya kiafya. Amepanga kuendelea kutoa msaada kwa kufanya kazi za kuongoza,akifanya kazi akiwa nyumbani. 
SOURCE ; BBC