Thursday, March 28, 2019

Ndege ya Serikali mbioni kubeba abiria, yapakwa rangi kwa Sh5milioni



Dar es Salaam. Rais John Magufuli amesema ndege ya Serikali aliyoagiza ipelekwe Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) na kuanza kusafirisha abiria inakamilisha upakaji rangi kwa Sh5 milioni tofauti na Sh260 milioni zilizotajwa na wataalamu.
Rais Magufuli amesema wataalamu walishauri ndege hiyo ikapakwe rangi, kuandika maneno, na kuchorwa Twiga nje ya nchi wakati jambo hilo linawezekana kufanyika nchini.
Akizungumza Ikulu jijini Dar es Salaam leo Machi 28, 2019  baada ya kupokea taarifa ya Takukuru na kumuapisha Balozi wa Cuba, Valentino Mlowola, Rais Magufuli amesema bado suala la rushwa ni tatizo.
 “Nchi hii ni hatari, kuna wajuaji wengi katika nchi hii, kuna maajabu mengi yanafanyika katika nchi hii,” amesema Rais Magufuli.
Akitoa mfano wa ndege, Rais Magufuli amesema aliposema ndege ya hiyo ipelekwe ATCL kuanza kusafirisha abiria, wataalamu walipokea na suala likawa kubadilisha maneno na twiga.
Amesema walimwambia kuwa suala hilo haliwezi kufanyika nchini na kutafutwa nchi tatu ambako, ndege hiyo ingeenda kupakwa rangi.

No comments:

Post a Comment