Wednesday, February 20, 2019

Alichokisema Jenerali Ulimwengu kuhusu Magufuli

Muasisi wa Kampeni ya ChangeTanzania, Maria

Muasisi wa Kampeni ya ChangeTanzania, Maria Sarungi akibadilishana mawazo na Mwanahabari Mkongwe, Jenerali Ulimwengu (katikati) pamoja na Mchora Katuni, Masoud Ally wakati wa mjadala kuhusu haki na wajibu wa rai ulifanyika jijini Dar es Salaam jana. 
Dar es Salaam.  Mwandishi wa habari mkongwe nchini Tanzania, Jenerali Ulimwengu amempongeza Rais John Magufuli kwa hatua mbalimbali anazochukua za kuwaletea maendeleo wananchi.
Hata hivyo, amemshauri mkuu huyo wa nchi kuachia jukwaa la  wananchi kuhoji na kutoa mawazo mbadala juu ya uwajibikaji na utekelezaji wa masuala yanayohusu maendeleo yao.
Ametoa kauli hiyo leo Jumatano Februari 20, 2019 katika kongamano la ‘Wenye Nchi ni Wananchi’ lililoandaliwa na Jukwaa la Tanzania yenye Mabadiliko.
 “Huwa sipendi sana kumsifu (Rais Magufuli) lakini kuna mambo mengi sana ambayo amefanya kwa uthubutu, wakati mwingine anakosea lakini anathubutu angalau, anachohitaji ni kusikiliza zaidi watu wanamwambia nini pale ambapo tunadhani amekosea,” amesema.
“Watu wanayo nia njema ya kumsaidia Rais lakini wakati mwingine anaonekana kama hasikilizi sawasawa, lakini angalau kwa uthubutu anao.”

No comments:

Post a Comment