Tuesday, August 13, 2019

PROFESA KABUDI; Zimbabwe kuondolewa vikwazo vya kiuchumi

Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri SADC, Profesa

Dar es Salaam. Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Profesa Palamagamba Kabudi amekabidhiwa rasmi  uenyekiti wa baraza la mawaziri la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kugusia nchi ya Zimbabwe kuondolewa vikwazo vya kiuchumi.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo Agosti 13, 2019 mbele ya Sekretarieti ya SADC, na Profesa Kabudi kuchukua nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na naibu waziri mkuu na waziri wa mambo ya nje wa Namibia,  Netumbo Nandi-Ndaitwah.
"Katika kipindi chetu tutahakikisha jumuiya ya kimataifa kuondoa vikwazo vya kiuchumi Zimbabwe. Lazima viondolewe  kwa kuwa kiongozi aliyekuwepo ameshaondoka madarakani na wananchi wanaendelea vizuri kwa sasa,” amesema Profesa Kabudi.
Akizungumza baada ya kukabidhiwa, Profesa Kabudi amesema  Tanzania katika kipindi hicho cha mwaka mmoja wa uongozi wake, itatekeleza kauli mbiu ya maendeleo shirikishi ya viwanda, kuongeza ajira pamoja na kusimamia kwa weledi masuala ya watoto, wanawake na afya.
"Tutazingatia suala la maendeleo endelevu na kuhakikisha tunaongeza viwanda, ajira pia asilimia 60 ya raia katika nchi 16 za SADC ni vijana hivyo lazima kuhakikisha tunaendeleza ajira," amesema.
Profesa Kabudi amesema suala muhimu kwa sasa ni kuhakikisha Kiswahili kinakuwa lugha rasmi ya SADC kwa kukuza lugha hiyo ambayo kwa sasa ni ya Tisa duniani.

MSD yawakabidhi shehena ya malori Muhimbili



Dar es Salaam. Bohari ya Dawa (MSD) nchini Tanzania imekabidhi dawa, vifaa na vifaa tiba kwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), kwa ajili ya kuwahudumia majeruhi wa ajali ya moto waliohamishiwa hospitalini hapo kutoka mkoani Morogoro.
Kwa mujibu wa MSD, makabidhiano hayo ya dawa ni mwitikio wa maombi ya dharura yaliyoombwa na MNH kwa ajili na majeruhi hao.
Majeruhi hao ni wale walionusurika katika ajali ya lori la mafuta ya petroli lililoangika kisha kulipuka eneo la Msamvu Mkoa wa Morogoro Jumamosi iliyopita ya Agosti 10, 2019 ambapo hadi jana Jumatatu jioni, waliokuwa wamefariki kutokana na ajali hiyo ni 75 na majeruhi zaidi ya 50.
Meneja wa MSD, Kanda ya Dar es Salaam, Celestine  Haule amesema mpaka leo Jumanne Agosti 13,2019 jumla ya shehena ya malori matano yameshakabidhiwa Muhimbili zikiwemo dawa muhimu zinazotumika kwa ajili ya kuokoa maisha ya majeruhi hao.
Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu amesema malori ya shehena za dawa, vifaa na vifaa tiba yalikabidhiwa jana Jumatatu na leo wanatarajia kupeleka dawa zingine.

Sunday, August 11, 2019

Ajari Morogoro Waliofariki waongezeka wafikia 71

Image result for ajali morogoro


Dar es Salaam. Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema idadi ya watu  waliofariki dunia katika ajali ya moto iliyotokea jana mkoani Morogoro imeongezeka kutoka 69 hadi 71.
Ajali hiyo imetokea jana Jumamosi Agosti 10, 2019 katika mtaa wa Itingi, Msamvu barabara ya Morogoro-Dar es Salaam baada ya lori la mafuta kupinduka na kuwaka moto muda mfupi baada ya watu kuanza kuchota mafuta.
Majaliwa ametoa kauli hiyo leo Jumapili Agosti 11, 2019 wakati akitoa taarifa fupi ya ajali hiyo katika ibada ya kuaga miili ya waliopoteza maisha iliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari  Morogoro.
“Vifo ni  71 na  majeruhi 59 hadi hivi sasa, hapa Morogoro wapo majeruhi 16 na hali zao zinaendelea vizuri kwa kuwa wanaweza kujieleza. Muhimbili kuna majeruhi 43 ambao wanaendelea na matibabu, hivyo tuendelee kuwaombea majeruhi hawa ili afya zao ziendelee kuimarika,” amesema Majaliwa.
Amewashukuru wananchi waliojitokeza kutoa michango mbalimbali ikiwemo taasisi ya Islamic Foundation, Benki ya NMB, CRDB na kampuni ya Tumbaku ya TLTC kwa mchango wao.
“Naendelea kumshukuru kila mmoja anayejitokeza katika kutoa mchango wake, nawashukuru sana kwa mchango wenu mkubwa tunauhitaji mkubwa katika eneo hili,” amesema Majaliwa.
Miili hiyo itazikwa katika makaburi ya kola mkoani Morogoro.

Thursday, August 8, 2019

Ubalozi wa Marekani na Wingereza Tanzania kwa pamoja watoa Tamko kuzorota kwa haki za raia kisheria nchini Tanzania

Image may contain: text

Serikali ya Tanzania yatangaza neema kwa wakulima wa korosho, mbaazi

Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa


Lindi. Serikali ya Tanzania imewaondoa hofu wakulima wa zao la korosho juu ya upatikanaji wa masoko kwa kusema lipo la uhakika na masuala yaliyotokea mwaka 2018 ilikuwa ni kwa masilahi ya kulinda wakulima ili kupata bei inayolingana na hadhi na gharama za uzalishaji.
Pia, imewahakikishia wakulima uhakika wa soko la mbaazi na kwamba mwaka 2019 litakuwa nzuri kwani tayari Serikali imefanya mazungumzo na India hivyo kutakuwa na mabadiliko tofauti na miaka iliyopita.
Akizungumza jana Alhamis Agosti 8,2919, Naibu Waziri wa Kilimo, Omari Mgumba alisema mpaka kufikia jana korosho zote zilizokuwa maghalani tayari zimepata mnunuzi na ndani ya muda mchache maghala yote kuanzia kusini hadi Dar es Salaam yatakuwa matupu.
“Hilo ni kuonyesha tumepata mahitaji makubwa ya mnunuzi ya korosho zetu, mahitaji tuliyoyapata hayakidhiwi na korosho tulizo nazo, ndiyo maana inaonyesha dalili hata korosho za msimu huu zitakuwa na soko kubwa na zitanunuliwa kwa bei stahiki kwa sababu tunajua korosho yetu ni bora lakini wakati wa kuzalisha ndio wazalishaji wakubwa duniani,” alisema Mgumba
Alisema korosho ya Tanzania inauzika na wanaopotosha kwamba korosho inaharibika sio kweli na ziko katika hali nzuri iliyoridhisha wanunuzi na kutoa bei ambayo Serikali imeridhika nayo.
Hata hivyo,  aliwataka wakulima wa mikoa ya kusini kufanya mgawanyo wa kilimo cha mazao mbalimbali kwa sababu yanapishana msimu tofauti na korosho ambayo ikishapandwa mkulima anaweza kuvuna kwa miaka mingi.
“Lazima tujielekeze na kwenye mazao mengine yatatuongezea kipato, tuongeze juhudi kwenye kilimo cha ufuta soko liko kubwa na nyinyi wenyewe ni mashahidi, tuongeze juhudi katika mbaazi na mwaka huu soko litakuwa nzuri tumeshazungumza na wenzetu wa India wamekubali kununua na soko litafunguka mtaona tofauti na miaka miwili iliyopita,”alisema Mgumba
Mkuu wa mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa alizitaka taasisi zilizoshiriki maonyesho hayo kuendelea katika maeneo hayo ili kuendelea na uzalishaji wa mbegu bora pamoja na kutoa mafunzo kwa wakulima na wafugaji.
“Nimeona kazi iliyofanywa na wataalamu wetu, mikoa ya Lindi na Mtwara tunataka kazi mlizozionyesha katika maonyesho haya muendelee nazo kwa mwaka mzima, Naliendele, Magereza na JKT wameniambia wataendelea kuwepo,hivyo niwasihi wananchi kutumia fursa hii kupata mbinu za kisayansi, teknolojia na ubunifu kutoka kwa taasisi husika kama ni kilimo, uvuvi au ufugaji kwa maslahi ya kuinua uchumi wao kama mtu mmoja mmoja na Taifa,” alisema Byakanwa
Mtafiti wa kilimo na mkaguzi wa mbegu kutoka taasisi ya kuthibiti ubora wa mbegu (TOSCI), Neema Yohana alisema baadhi ya wakulima wamekuwa wakiuziwa mbegu bandia na kuwaletea mazao yasiyo mazuri huku akiwataka kutumia ofisi hiyo na maonyesho yanayofanyika kujua namna ya kutambua mbegu bora na kuepukana na bandia.
“Mbegu bandia zimekuwepo baadhi ya maeneo kwa wakulima kudanganywa kwa sababu hawafahamu wanatakiwa kununua mbegu kwenye maduka ya watu waliosajiliwa na TOSCI zinakuwa zimethibitishwa ubora na pia zina lebo ya TOSCI na wanaponunua wadai risiti ili kuepukana na mbegu bandia lakini kusaidiwa ikitokea ameuziwa mbegu bandia,” alisema Yohana


Wafanyabiashara SADC washawishika kuwekeza Tanzania

Wananchi wakiwa kwenye banda la Brela kwenye


Dar es Salaam. Wafanyabiashara katika Jumuiya ya Maendeleo ya kusini mwa Afrika (SADC) wamejitokeza kwa wingi katika banda la maonyesho la Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini Tanzania (BRELA) kwa lengo la kusajili kampuni na kuwekeza katika viwanda.
Akizungumza na Mwananchi jana Alhamisi Agosti 8, 2019 Jijini Dar es Salaam nchini Tanzania ikiwa ni siku ya mwisho ya maonyesho ya bidhaa katika wiki ya viwanda kwa Nchi 16 za jumuiya hiyo, Mwandamizi Msajili msaidizi, Angela Kimario alisema tangu kuanza kwa maonyesho hayo wamejitokeza wageni kutoka Zimbabwe, Afrika Kusini na Malawi.
“Jana (juzi) nilipokea wafanyabiashara wa Malawi, Afrika Kusini watatu na wengi walikuwa wafanyabiashara wa Zimbabwe, baada ya maelezo yetu wameonyesha nia ya kuja kuwekeza katika viwanda na kusajili kampuni, takwimu sina kwa sasa,” alisema Angela.
Hata hivyo, Angela alisema sheria mbili; sheria ya kampuni ya mwaka 2002 na Sheria ya Taifa ya Viwanda inayohusika na usajili na utoaji wa leseni ya mwaka 2002 hazijaweka vipaumbele kwa nchi 16 za Jumuiya hiyo
“Kwa hiyo taratibu za kusajili kampuni zinabakia kuwa zilezile kwa yeyote anayetoka nchi za SADC au ndani ya SADC, kazi kubwa inafanywa na watu wa Kituo cha uwekezaji , hao ndiyo wanaweza kuwa na vipaumbele zaidi katika eneo hilo,” alisema Angela.

Sunday, August 4, 2019

Bodaboda Kilimanjaro watangaza kuiunga mkono CCM 2020

Image result for bodaboda ccm


Moshi. Chama cha Wamiliki na Waendesha Bajaji na Bodaboda Mkoa wa Kilimanjaro (CWBK), kimetangaza kumuunga mkono Rais wa Tanzania  John Magufuli katika uchaguzi mkuu utakaofanyia 2020.
Hata hivyo, chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimedai kushtushwa na msimamo huo na kueleza kuwa ndani ya kundi kuna ambao ni wana CCM, wafuasi wa upinzani na wasio na vyama.
Chama hicho chenye wanachama 4,500 kimetangaza msimamo huo mwishoni mwa wiki katika mkutano wa wamiliki na waendesha bajaji na pikipiki, uliofanyika ofisi za CCM mkoa Kilimanjaro.
Msimamo huo ulitolewa kupitia risala yao kwa mgeni rasmi wa mkutano huo ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola ambaye pia ni Mbunge wa Mwibara kupitia CCM.
Awali risala hiyo ilikuwa isomwe na mwenyekiti wa chama hicho, Bahati Nyakiraria lakini baadhi ya wanachama wakapaza sauti wakipinga, ndipo iliposomwa na Katibu wa UVCCM mkoa, Asia Halamga.
“Tunaomba umpelekee Rais Magufuli salamu zetu za dhati kuwa tunamuunga mkono kwa kazi kubwa anayofanya ya kuwaletea watanzania maendeleo,” inaeleza sehemu ya risala hiyo.

 “Sisi wasafirishaji tunafurahi kwa kutuletea treni ya mizigo na abiria kwani kwetu itakuwa fursa ya kuongeza kipato kwa kutoa huduma za usafiri pale kituoni. Mtoe wasiwasi (Rais) kuhusu chaguzi zinazokuja za Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu. Tutakiunga mkono CCM  kwani kinatetea wananchi wake.”
katika mkutano huo ulihudhuriwa pia na mwenyekiti wa CCM Mkoa Kilimanjaro, Patrick Boisafi na Katibu wa mkoa, Jonathan Mabhia, Lugola alitatua papo kwa hapo, kero mbalimbali za kundi hilo.
Miongoni mwa kero alizoelezwa Lugola ni pamoja na madereva wa Bajaji na Bodaboda kukamatwa  na kupigwa faini ya kuanzia Sh30,000 kwa makosa yanayohitaji kupewa tu elimu.
Kero nyingine ni madereva kukamatwa na kuwekwa mahabusu kwa kushindwa kulipa faini papo hapo, kero ambayo Waziri aliitolea maamuzi kuwa wanapaswa kuandikiwa faini na kulipa ndani ya siku saba.
Mojawapo ya kero aliyoitatua papo hapo ni kuagiza kurejeshwa kwa vituo viwili vya Bajaji vya Kwa Sharifu soko la Mbuyuni na Agakhan karibu na kituo kikuu cha mabasi vilivyofutwa kinyemela.
Pia,  alimwagiza kamanda wa Polisi mkoa Kilimanjaro, Hamis Issah aliyekuwepo katika mkutano huo, kufanyia kazi malalamiko ya rushwa kwa trafiki watatu waliotajwa katika mkutano huo kuwa vinara.
“Matatizo mengi mliyowasilisha kwangu ni yale yanayosababishwa na Halmashauri zenu mbili. Kama ni matatizo ya maegesho viongozi wako hapa kuanzia mstahiki Meya na madiwani,” amesema Lugola.
“Hawa ndio wamewafanya watumwa ndani ya nchi yenu. Fanyeni matengenezo sasa na ni CCM pekee ndio kuna hewa ya Oksijeni. Acheni kutumia hewa ya ukaa mtakufa,”alisisitiza Waziri Lugola.
Waziri Lugola aliwaonya watendaji wa taasisi za Serikali wanaowawekea vikwazo wamili na waendesha Bodaboda na Bajaji, akisema dawa yao inachemka kwani Rais Magufuli hataki mambo hayo.
Chadema Kilimanjaro wanena
Katibu wa Chadema mkoa Kilimanjaro, Basil Lema amesema watamuandikia barua msajili wa Asasi za Kiraia kuhoji uhalali wa CWBK kutoa matamko ya kisiasa ambayo si malengo ya chama hicho.
“Kiukweli tumeshtushwa sana na msimamo ulitolewa Ijumaa. Hatuamini kulikuwa na consensus (makubaliano) katika kuandika hotuba hiyo. Humo ndani kuna wana CCM na upinzani,” amesema.
Lema amedai CCM kimeishiwa mbinu ndio maana kimeamua kucheza rafu kwa kumuita Waziri Lugola kwenda Kilimanjaro kwa kodi ya watanzania, lakini akaenda kufanya kazi za kukiimarisha CCM.
Kwa mujibu wa Katibu hiyo, wanafahamu sababu za CCM kuamua kushika kundi hilo ni kutokana na kuzidiwa na upinzani na kufananisha na mtu anayezama hivyo hata akiona unyoya anaushika.